Taarifa iliyotolewa na Ikulu ya Misri mjini Cairo, inaeleza kwamba Rais el-Sisi na Sullivan walizungumzia pia suala la ujenzi wa Ukanda wa Gaza, mvutano kuhusu bwawa la Ethiopia kwenye mto wa Blue Nile Gerd uhusiano kati ya Marekani na Misri na hali nchini Tunisia Yemen na Iraq.
Mwanamke asiyefahamika katika siasa za Tunisia, Najla Bouden ateuliwa waziri mkuu mpya, jambo linalowafurahisha wengi, lakini wachambuzi wahoji ikiwa ataweza kukabiliana na matatizo makubwa ya kisiasa yanayoikumba Tunisia.
Uchunguzi huo umegundua kwamba mkataba uliotolewa kwa kampuni ya Digital Vibes haukuwa sahihi na maafisa wa juu wamefaidika kutokana na baadhi ya pesa zilizolipwa na kampuni hiyo.
Maelfu wengine wamekwama kwenye mji wa kusini wa Tapachula karibu na mpaka wa Guatemala wakati wakisubiri majibu kutokana na maombi yao ya hifadhi nchini Mexico kutoka kwa maafisa wa uhamiaji wa taifa hilo.
Kundi la kijeshi lililofanya mapinduzi kwenye taifa la Afrika magharibi la Guinea Jumanne limetoa wakaraka unaoahidi kurejesha taifa hilo kwenye utawala wa kiraia.