Rais mpya wa Kenya William Ruto alisema Jumatano kwamba nchi hiyo ya Afrika Mashariki imevunja uhusiano wa kidiplomasia na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kiarabu ya Sahrawi (SADR) inayozozaniwa katika Sahara Magharibi, baada ya kufanya mazungumzo na Morocco.
Wakati visa vya maambukizi ya Monkeypox vikiendelea kushuka kwenye mataifa ya Ulaya pamoja na Marekani, wataalam wa sayansi wanasema kwamba sasa ni wakati wa kuweka kipaumbele cha upatikanaji wa chanjo dhidi ya maradhi hayo barani Afrika.
Mkuu wa Shirika la Afya Duniani, WHO, anasema idadi ya vifo vilivyotokana na Covid 19 wiki iliyopita ilikuwa ndiyo ndogo zaidi iliyoripotiwa katika janga hilo tangu mwezi Machi mwaka 2020.