Waziri Ummy Mwalimu atoa siku 7 kwa vyombo vya usalama kuchunguza vifo vya wanafunzi watatu Mpwapwa
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Ummy Mwalimu ametoa siku 7 kwa vyombo vya Ulinzi na Usalama kuchunguza vifo vya wanafunzi 3 waliofariki kwa kufunikwa na kifusi katika Shule ya Msingi Mbori, Kata ya Motondo Wilayani Mpwapwa.
Wakati huo huo Mhe. Ummy amemuagiza Mkuu wa Mkoa wa Dodoma kuwaondoa Walimu wote wa shule ya Msingi Mbori kupisha uchunguzi unaondelea.
Waziri Ummy ametoa kauli hiyo wakati aliposhiriki kuaga Miili ya wanafunzi 3 waliofariki kwenye ajali ya kufukiwa na Mchanga katika shule ya Msingi Mbori tarehe 27.07.2021.
Vifo vya vigogo vyatikisa Januari | Jisomee Habari za Udaku, Siasa, Mapenzi na Michezo udakuspecially.com - get the latest breaking news, showbiz & celebrity photos, sport news & rumours, viral videos and top stories from udakuspecially.com Daily Mail and Mail on Sunday newspapers.