Barcelona ina matumaini ya kumsajili kiungo wa kati wa Ufaransa na Man United Paul Pogba katika uhamisho wa bila malipo msimu ujao iwapo mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 28 ataamua kutotia saini kandarasi mpya na Man United , ijapokuwa watakabiliwa na ushindani mkubwa kutoka klabu za PSG , Juventus na Real Madrid . (Fichajes - in Spanish)