Soko Kuu mjini Mombasa lateketea kwa moto
11 Julai, 2021
Shirikisha
share
Print
Soko maarufu la Marikiti mjini Mombasa nchini Kenya limepata hasara kubwa kutokana na moto ambao ulilikumba soko hilo Jumamosi usiku kuamkia Jumapili.
Wafanya biashara katika soko maarufu la Marikiti mjini Mombasa wamepata hasara kubwa baada ya moto mkubwa kushuhudiwa usiku wa Jumamosi kuamkia Jumapili
Hakuna ripoti za maafa wala majeruhi kufikia sasa huku juhudi za kuzima moto huo zikiendelea.
Magari ya zima moto kutoka kitengo cha serikali za ugatuzi wakishirikiana na polisi wako kwenye tukio wakijaribu kudhibiti hali.
Wakati huu ambapo kuna sharti la kutotoka nje wakati wa usiku kwa sababu ya kuzuia maambukizi ya virusi vya corona, baadhi ya wakaazi wa maeneo ya karibu wako nje kushuhudia moto huo na wengine wakitoa msaada wa kudhibiti moto.
Nani Kachoma Soko la Kariakoo, Mashuhuda Walalamika vifaa Duni
udakuspecially.com - get the latest breaking news, showbiz & celebrity photos, sport news & rumours, viral videos and top stories from udakuspecially.com Daily Mail and Mail on Sunday newspapers.
Soko Kuu Mjini Mombasa Lateketea kwa Moto
udakuspecially.com - get the latest breaking news, showbiz & celebrity photos, sport news & rumours, viral videos and top stories from udakuspecially.com Daily Mail and Mail on Sunday newspapers.