Upinzani waomba nafasi zaidi ya kisiasa, Tanzania
2 Julai, 2021
Shirikisha
share
Print
Viongozi wa upinzani pamoja na wanaharakati wa Tanzania Alhamisi wamefanya kikao cha kuomba serikali kufanya marekebisho kwenye katiba ili kuongeza uhuru wa kisiasa nchini. K
ikao hicho kilichopewa jina Katiba Day, kimefanyika muda mfupi baada ya rais mpya Samia Hassan kuomba watanzania kumpa nafasi ya kufufua uchumi kwanza kabla ya kufanya marekebisho ya katiba.
Kikao cha Alhamis kinaonekana kuchochewa na matamshi ya rais Hassan hapo Jumatau wakati alipofanya kikao cha kwanza na wanahabari. Kiongozi huo aliomba watanzania kumpa nafasi ya kufufua uchumi kwanza kabla ya kuondoa marufuku iliowekwa dhidi ya mikutano ya kisiasa pamoja na kurejea mchakato uliositishwa kuelekea marekebisho ya katiba.
Je Rais Samia ni mvinyo mpya kwenye chupa ya zamani au chupa mpya yenye mvinyo wa zamani? bbc.com - get the latest breaking news, showbiz & celebrity photos, sport news & rumours, viral videos and top stories from bbc.com Daily Mail and Mail on Sunday newspapers.